Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Friday, June 20, 2014

   
Uganda imepitisha mswada unaopinga mapenzi ya jinsia moja.
Iwapo Rais Yoweri Museveni ataidhinisha sheria hiyo inamaanisha atakayepatkana na hatia atahukumiwa kifungo cha maisha gerezani.
Mswaada huo uliopitishwa na bunge siku ya Ijumaa halikadhalika inasema mtu yeyote aliye na taarifa za watu wanoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kushindwa kuripoti habari hizo kwa maafisa wa polisi atafungwa gerezeni maisha.
Wakati hu huo bunge hilo hilo la Uganda siku ya Alhamisi liliidhinisha mswaada unaopiga marufuku maonyesho ya picha za chafu.
Mswada huo unaharamisha kitu chochote kitakachoonyesha sehemu nyeti kama vile matiti, mapaja, makalio au tabia yoyote inayozua uchu wa mapenzi.
Kufuatia kuoitishwa kwa sheri ahiyo wanaharakati wa wapenzi wa jinsia moja, mawakili na wansiasa wamewasilisha kesi mahakamani nchini Uganda kupinga sheria mpya dhidi ya mapenzi ya jinsia moja nchini humo.
Wanaharakati hao, wanasema kuwa sheria hiyo inakiuka katiba ya Uganda na kuendeleza ubaguzi na kukandamiza uhuru wa kujieleza.
Sheria hiyo ilitiwa saini na Rais Yoweri Museveni mwezi jana na imelaaniwa vikali na jamii ya kimataifa.
Marekani imeiwekea Uganda vikwanzo kuhusina na sheria ya wapenzi wa jinsia moja.
Rais wa Marekani Barack Obama ameitaja sheria hiyo kama hatua ya ukandamizaji kwa waganda na nchi kadhaa tayari zimetishia kuinyima Uganda msaada.

0 comments:

Post a Comment