Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Wednesday, November 26, 2014


Rappa toka pande za Miami,Rick Ross ameushtua ulimwengu kwa kupunguza mwili kwa kiasi kikubwa na kubadili muonekano.Ross amepunguza karibia ya pound 200 kwani alikuwa na pound 300 na sasa anakaribia pound 100.

Ross ambaye alishawahi kupoteza fahamu mara mbili ndani ya siku moja kwa matatizo ya afya kutokana na mwili mkubwa,akiongea na waandishi wa habari amesema,amefanikiwa kupunguza mwili kwa kula mlo alioelekezwa,kufanya kazi muda mwingi zaidi na mazoezi.Ross amesema hata afya inahitaji nidhamu.
Ross, 37, amesema anaendelea kufanya kazi za nguvu na muda mrefu haswa katika shughuli zake za kimuziki na hivi karibuni ameachia albamu yake ya saba na ya pili mwaka huu "Hood Billionaire," baada ya kuachia mwezi March albamu ya  "Mastermind," ambayo ilifika hadi namba 1 katika chati za Billboard albamu mia 2 bora .

0 comments:

Post a Comment