Justin Bieber na Usher wamefunguliwa mashtaki ya madai ya kunakili wimbo na muimbaji wa R&B Devin Coperland aka De Rico.
De Rico katika mashtaka yake amedai mastaa Bieber na Usher wamenakukili sehemu kubwa ya wimbo wake kuanzia mtindo,melody,mdundo hadi jina "Somebody to Love."De Rico alifungua mashtaka mara ya kwanza katika mahakama ya mwanzo mwaka 2014 chini ya hakimu Arenda Wright ambapo madai hayo yalitupiliwa mbali baada ya hakimu kutoridhishwa na ushahihidi uliotolewa.Kesi hiyo imepitiwa upya na kukutwa kuna ukweli baada ya jopo la wanasheria kuzisikiliza nyimbo hizo na kuona kuna muendano hivyo jana (June 18) waliamuru kesi hiyo kusikilizwa upya.
De Rico amesema anataka kulipwa kiasi cha dolla millioni 10 kama fidia ya usumbufu na uharibifu wowote uliojitokeza na shemu ya faida waliyojipatia mastaa hao kupitia wimbo huo
Tunangoja kusikilizwa kwa kesi hiyo ambayo bado haijapangiwa tarehe.
Friday, June 19, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment