Rapa Drake ametangaza kusitisha mpango wa kukutana,kusalimiana na kupiga picha na mashabiki katika ziara yake ya “Summer Sixteen,” .
Ziara ya “Summer Sixteen Tour” ambayo atakuwa na rapa Future,imetangazwa kuanza July 20 huko Austin.
Mashabiki walionunua tiketi za ziara hiyo za VIP kwa dola 1,000 ili waweze kupeana mikono na kupiga picha na Drake,wametangaziwa kurejeshewa dola 300 ila watakaa VIP.
Upande wa waandaaji wa maonyesho hayo hawajatoa ufafanuzi juu ya nini kimepelekea kusitishwa kwa mpango huo wa Drake kusalimiana na kupiga picha na mashabiki ila tu wameomba radhi na wametoa utaratibu jinsi watakavyorejesha pesa.
Thursday, June 23, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment