Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Thursday, February 26, 2015

Image result for marijuana in washington dc

Mji mkuu wa Marekani Washington DC umehalalisha utumizi wa Bangi.Hatua hii ya Washington inafuatia ile ya jimbo la Colorado, Alaska na Washington state ya kuhalalisha matumizi ya mihadarati kwa starehe.
Mpango huo umekubalika na wananchi wengi katika kura ya maoni iliyopigwa Novemba mwaka jana lakini maafisa nchini humo wametofautiana na wabunge wa Republican ambao ni wengi bungeni uliosababishwa kusitisha eneo hilo kuidhinisha mbinu za kudhibiti na kutoza kodi mhadarati huo.Sheria hiyo mpya itaanza kutumika kuanzia saa tano usiku wa Alhamisi na hivyo mtu yeyote atakayekuwa akimiliki bangi kisiri atakuwa huru kuivuta bila hofu ya kukamatwa..
Sheria hiyo mpya hata hivyo imezua tofauti baina ya Meya wa mji huo na bunge la Congress.
Weneyji wa mji huo wenye umri unaozidi miaka 21 watakuwa huru kumiliki gramu 56 ya Bangi na wanauwezo wa kuipanda majumbani mwao.
Katika Barua iliyoandikwa na wajumbe wa bunge hilo la Congress,Meya wa Washington Muriel Bowser ameonywa kuwa sheria za jimbo zinakiukwa iwapo sheria hiyo maarufu itaanza kutekelezwa.Wajumbe hao wanadai kuwa kulingana na sheria maalum iliyopitishwa na Bajeti ya taifa Kuhalalishwa kwa bangi ni haramu.
Bi Bowser hata hivyo anaendelea kushikilia kukutu kuwa walifwata kanuni zote zilizowekwa.



0 comments:

Post a Comment