Surprise! Chris Brown ni baba sasa.Taarifa toka katika mtandao wa TMZ,zimesema,star huyo wa R&B ni baba wa mtoto wa kike wa miezi 9.
Mama wa mtoto huyo anafahamika kwa jina la Nia (31) ambaye alikuwa mwanamitindo na walikuwa watu wa karibu na Chris Brown kwa miaka mingi.
Nia na Chris wameripotiwa kuwa katika maelewano mazuri japo si wapenzi na taarifa zaidi zinadai Chris Brown alifurahia habari njema za kuwa baba.
Alipofanyiwa mahojiano na kipindi cha “The Breakfast Club” mwezi uliopita,Chris aliongeea swala la kuwa muaminifu sana katika mahusiano yake na mpenzi wake Karrueche na kusema anampenda sana japo anapenda kula bata na mabinti wakimzunguka.
0 comments:
Post a Comment