CNN imeripoti kikundi cha mabinti toka mji wa Alabama huko marekani walifikia kuamua kuuchukua ugomvi wao na binti mwingine kutoka katika mtandao wa kijamii mpaka kukutana naye na kuzipiga kavukavu huko Birmingham park huku wakiwa na mawazo ya kurekodi mpambano huo ili baadaye wautume mitandaoni.
Wakati mpamban baina ya mabinti hao ukiendelea ghafla wakatokea wanaume na kuanza kufyatua oyo risasi kwa nia ya kusimamisha ugomvi huo kitendo kilichopelekea kukatisha maisha ya binti mwenye umri wa miaka 14 aliyetambulika kwa jina la Kierra’onna Rice na wengine kupatwa na majeraha makubwa.
Wana usalama wamesema mmoja kati ya washukiwa wa mauaji alikuwa mpenzi wa mmoja kati ya mabinti waliokuwa wakigombana.
0 comments:
Post a Comment