Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Wednesday, June 29, 2016



Ice Cube and John Legend
Nyota mpya kuwekwa mwakani katika sehemu maarufu duniani ya Hollywood Walk of Fame .
Wahusika na uwekaji wa nyota hizo za heshima,The Hollywood Chamber of Commerce and Walk of Fame wametangaza kuongeza nyota maka 2017,kwa masta Ice Cube, John Legend, na New Edition .
 Hollywood Walk of Fame ni njia ya miguu iliopo mjini Hollywood Boulevard na Vine Street huko Hollywood, Los Angeles, California, Marekani, ambayo hutumiwa kama sehemu ya maonyesho ya burudani. Imetiwa zaidi ya nyota yenye-pembe tano 2,000 ikiwa na majina sio ya binadamu mashuhuri peke yake bali hata yale ya wahusika wa katuni pia wamepewa nyota kwenye Hollywood kwa mchango wao katika tasnia ya burudani.
Nyota za kwanza zilitolewa mnamo mwezi wa Septemba katika mwaka wa 1958 na kuwekwa kwenye njia ya miguu kwenye kona ya kaskazini mwa Hollywood Blvd. na Highland Ave.
Sambamba na mastaa  Ice Cube, John Legend, na New Edition pia wametajwa *NSYNC, Clarence Avant, na late Selena.
Upande wa filamu wametajwa Amy Adams, Jason Bateman, Goldie Hawn, Dwayne Johnson, Chris Pratt, Brett Ratner, Ryan Reynolds, George A. Romero, Mark Ruffalo,na Rita Wilson.
Television stars ni Tyra Banks, Andre Braugher, Ken Corday, Lee Daniels, Hugh Laurie, Eva Longoria, Wolfgang Puck, Keri Russell, Haim Saban, George Segal, Sarah Silverman,na Jeffrey Tambor.
Pia wapo mastaa upande wa radio ambao wote kwa ujumla watasimikiwa nyota zao katika sherehe maalumu ya usimikaji mwaka 2017 .
Hollywood Chamber of Commerce walianzisha mradi huo kama kivutio cha watalii ambao watatembelea  Hollywood kuona nyota za wasanii wanaowapenda, directors , producers nk.

0 comments:

Post a Comment