Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Tuesday, July 1, 2014

Nicki alionekana akirusha madongo kwa Iggy pale alipopewa nafasi ya kushukuru na kuongea nawatu wake baada ya kukabidhiwa tuzo ya Best Female Hip Hop Artist baada ya kujisema yeye ni spesho kwani anatunga na kuandika nyimbo zake mwenyewe ukimlinganisha na waimbaji wengine maarufu wanaopata mafanikio na kuingiza mkwanja kwa nyimbo za kuandikiwa.Niwzi alikuwa akimsema Iggy Azalea, 24 na entertainers wengine waliohudhuria tuzo hizo huko L.A Nokia Theater June 29.Watu makini wamemkosoa Nicki Minaji kwa kusema unaweza ukawa una kipaji na nyota na bado ukawaunaandikiwa.Iggy Azalea ameshawahi kumshirikisha nicki minaj katika wimbo Fancy.

stage name Iggy Azalea jina lake Amethyst Amelia Kelly (amezaliwa 7 June 1990),  ni muaustralia muimbaji,mwanamitindo aliyeahamia United States akiwa na umri wa miaka 16, na kujiingiza katika fani ya hip hop music,ambapo alifikia Miami,Florida, na kisha kuhamia Houston, Texas na Atlanta, Georgia.Iggy ameshafanya kazi na lebo mbalimbali zikiweo Virgin EMI,Def Jam,Mercury na sasa yupo Grand Hustler chini ya rappa T.I.

Katika maisha yake ya muziki Azalea amewataja marappa wa American waliomvutia afanye sanaa ya muziki kwa kuwataja mwanamama Missy Elliott na hayati Tupac Shakur kama ndiye haswa aliyemsukuma.

0 comments:

Post a Comment