Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Tuesday, May 20, 2014

 









bbc.co.uk/swahili/michezimeandika,Louis van Gaal ametangazwa kuwa kocha mpya wa Manchester United, huku aliyekuwa kocha wa muda Ryan Giggs akifanywa kuwa msaidizi wake.
Raiya huyo wa Uholanzi, ametia saini mkataba wa miaka mitatu, na atachukua usukani wa timu hiyo baada ya kuiongoza timu ya taifa ya Netherlands katika kombe la dunia litakalofanyika nchini Brazil.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 62 amewahi kushinda mataji na vilabu vya Ajax, Barcelona na Bayern Munich.Manchester United ilimfuta kazi David Moyes mwezi Aprili, miezi 10 tu baada ya kuchukua usukani baada ya kustaafu kwa Alex Fergurson, aliyekuwa mkufunzi wa timu hiyo kwa miaka 26.

Mataji ya kitaifa:
Ajax (1993-94, 1994-95, 1995-96),
Barcelona (1997-98, 1998-99),
Bayern Munich (2009-10)Klabu bingwa ulaya:
Ajax (1994-95)Kombe la Uefa:
Ajax (1991-92)
Gigs aliye na umri wa miaka 40 alichukua usukani kama mkufunzi wa muda katika mechi nne za mwisho wa msimu uliopita.
Alikutana na Van Gaal nchini Netherlands juma lililopita ili kuzungumza kuhusu hatima yake katika klabu hiyo,kama mmoja kati ya wakufunzi na wakati huo huo akiwa mchezaji.
United walimaliza wa saba katika ligi ya premier, baada ya waliokuwa mabingwa watetezi kushindwa na Manchester City, Liverpool na Chelsea.
Walishindwa kufuzu kucheza mechi ya vilabu bingwa wa Uropa kwa mara ya kwanza tangu mwaka wa 1995-96, na hawatacheza mechi zozote za kiropa kwa ujumla kwa mara ya kwanza kwa miaka 26 iliyopita.
Mchezaji mkongwe wa klabu hiyo Giggs, meneja wa Real Madrid Carlo Ancelotti na meneja wa Borussia Dortmund Jurgen Klopp walikuwa wamehusishwa na kazi hiyo, lakini Van Gaal ndiye aliyechaguliwa ili kuiongoza timu hiyo kurejea kileleni mwa ligi za premier na michezo ya Uropa
Kocha huyo mpya anatarajiwa kupewa pesa nyingi ili kuwasajili wachezaji wapya

0 comments:

Post a Comment