
Kutoka Queen Latifah mpaka Tupac
na mastar wengine wakubwa wa Hip Hop wamewekewa nyota maalumu katika Hollywood Walk of Fame na sasa taarifa zilizopo ni kwamba star wa Rap,pop na producer,Pharrell William naye kuwekewa nyota.
Taarifa toka kwa wahusika na uteuzi na uwekaji nyota huko Hollywood Walk of Fame chini ya mwenye kiti wake Maureen Schultz zimesema, Pharrell Williams atawekewa nyota ya pembe tano mwezi December tarehe 4.
Hollywood Walk of Fame ni njia ya miguu iliopo mjini Hollywood Boulevard na Vine Street huko Hollywood, Los Angeles, California, Marekani,
ambayo hutumiwa kama sehemu ya maonyesho ya burudani. Imetiwa zaidi ya
nyota yenye-pembe tano 2,000 ikiwa na majina sio ya binadamu mashuhuri
peke yake bali hata yale ya wahusika wa katuni pia wamepewa nyota kwenye
Hollywood kwa mchango wao katika tasnia ya burudani. The Walk of Fame
ni inajipatia fedha na Hollywood Historic Trust. Nyota za kwanza
zilitolewa mnamo mwezi wa Septemba katika mwaka wa 1958 na kuwekwa
kwenye njia ya miguu kwenye kona ya kaskazini mwa Hollywood Blvd. na Highland Ave.
Friday, November 28, 2014
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment