Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday
Posted by djnicotracktz
on 3/11/2015 03:44:00 AM
No comments
Mwaka 2013 watoto wa aliyekuwa muimbaji nguli wa marekani,Marvin Gaye,Nona, Frankie na Marvin Gaye III walifungua mashtaka kuhusu kuibiwa sehemu ya wimbo wa marehemu baba yao na kutengenezwa wimbo Blurred Lines ambao uliwaingizia dolla millioni 16million waimbajiP harrell, Thicke na rapper T.I.
Hukumu iliyotolewa jana march 11 imewataka Pharell na Robin Thicke kuilipa familia ya Marvin Gaye dolla millioni 7.4 kwa kunakili wimbo bila makubaliano na familia hiyo.
Mahakama imeamua kwamba familia hiyo ya Gaye italipwa dolla millioni 4 kama usumbufu na kuendesha kesi hiyo na dolla millioni 3.4 kama sehemu ya faida kutoka mapato ya mauzo ya wimbo huo ambapo mahakama imemtaka Robin Thicke ametakiwa kulipa dola 1.7 kutoka mfukoni mwake na Pharrell kulipa dolla millioni 1.6 toka mfukoni mwake.
0 comments:
Post a Comment