Raisi Barack Obama alikuwa katika mahojiano na kipindi cha "Jimmy Kimmel Live,mahojiano yanayoonyesha kama hakuna urafiki kati ya President
Barack Obama na rapper Kanye West.
Hivi karibuni West alialikwa kutoa hatuba katika chuo kikubwa cha Oxford University na moja kati ya mambo aliyosema ni kwamba yeye na raisi wa Marekani,Barack Obama ni watu wa karibu na wanawasiliana,huwa anampigia simu na kama haitoshi raisi huyo huwa anampigia hata katika simu ya nyumbani ya mezani kitu ambacho raisi Obama alikikanusha alipohojiwa katika kipindi cha "Jimmy Kimmel Live.Raisi Obama alisema,napenda muziki wake,ni m bunifu na anajua sana ila sina namba zake.
Obama ambaye hapo awali aliwahi kumita Kanye west mnafiki kufuatia tukio la kumvamia jukwaani Taylor Swift wakati akishukuru kufuatia kupata tuzo ya Grammy,amesema yeye na Kanye West hawajakutana zaidi ya mara mbili.Mara ya kwanza kukutana naye wakati akiwa seneta wa Chicago na mara ya pili ni katika sherehe kama miezi sita iliyopita.
0 comments:
Post a Comment