Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Monday, August 17, 2015


Muimbaji mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Diamond Platnum alihudhuria sherehe ya kuzaliwa ndugu yake,Rome Jones iliyofanyika jana August 16 katika ukumbi wa The House uliopo Masaki.
Romy Jones aalialika mastaa kibao akiwa ndugu yake,Diamond Platnums, na masta kibao kama Shilole,Nuh Mziwanda,Barnaba Classic,Jux,Vanessa Mdee,T.I,D,Q Chilla,Domokaya na mastaa wa fani mbali mbali wakiwamo madj kama Dj Zero wa Clouds,Dj Tas wa Magic Fm,Dj Ommy Crazy wa East Africa Fm,Dj Nicotrack,Dj Omy wa Maisha Club.
Sherehe hiyo ilijaa mbwembwe na burudani za hapa na pale kwani ukuachilia mbali burudani safi ya muziki pia wasanii wa muziki wa kizazi kipya walitumbuiza.Mbali na kutumbuiza,Diamond platnum alichukua nafasi hiyo kuwapaisha na kwashukuru wasanii waliomtangulia kwa kumfanya awe pale alipo.Sambamba na wengi aliowataja,Diamond aliwaongelea T.I.D na Q Chila kwanza aliwapongeza kitendo chao cha kumaliza tofauti zao na pia aliwataja kuwa wana mchango mkubwa sana kwake huku akimtaja Q Chila katika uimbaji na T.I.D katika kuvaa,kucheza na kushambulia jukwaa.

0 comments:

Post a Comment