Presenter/DJ at RadioOne stay with me "Dj Show" Monday to Friday

RadioOne Dar es salaam 89.7FM|Arusha 95.3FM|Tabora 98.1FM|Dodoma 100.8FM|Mwanza 102.9FM|Moshi 132.3KHZ|Morogoro 103.2MHZ|Tanga 106.3MHZ|Bukoba 92.1MHZ Home of Good Music Tanzania

Wednesday, September 16, 2015


 Baada ya kuonekana kumuunga mkono Tennis star Serena Williams kwa kumshanglia kwa nguvu katika mashindano ya mpira wa tennis ya U.S Open hivi karibuni,rappa Drake kwa mara nyingine ameoneka kumuunga mkono Serena baada ya kuhudhuria na kukaa siti za mbele kabisa katika maonyesho ya mitindo ya mavazi ya Serena Williams ikiwa kama sehemu ya maonyesho ya New York Fashion Week jana siku ya jumanne.
Wanamitindo walitembea jukwaa huku katika spika zikisiskika nyimbo mbali mbali za Drake zikiwemo “Hotline Bling,”“My Love” na “Ojuelegba,” aliyoshirikikishwa na msanii toka Africa,mnaijeria Wizkid.
Drake pia alionekana akiwa na Serena backstage akimpongeza kwa furaha na mabusu mkononi.

Drake pia alionekana amekaa siti za mbele na Anna Wintour ambaye ni editor in chief wa jarida la  Vogue baadaye picha hiyo ikatumwa mtandaoni ikiwa na caption “Me and bae.”

0 comments:

Post a Comment