Shabiki mmoja wa muziki amefungua mashataka kwa Chris Brown na timu yake kwa kile alichokisema walimchukulia kofia yake na hawakumrejeshea.
Shabiki huyo aliyefahamika kwa jina la Marq Stevenson amesema alimpatia kofia yake mmoja wa watu wa timu ya Chris Brown ili kofia yake isainiwe na muimbaji huyo lakini haikurejeshwa.Tukio hilo lilitokea mwaka 2015 katika onyesho la muziki huko Dallas, Texas.
Shabiki huyo aliyefahamika kwa jina la Marq Stevenson amefungua mshataka na kutaka Chris Brown na timu yake wamlipe kiasi cha dola za kimaekani 2,750 na kuchanganua kwamba dola 25 za manunuzi ya kofia,dolla 225 ya manunuzi ya tiketi ya inyesho na dola 2,500 za kujiliwaza kwani aanahisi amedharauliwa na kunyanyaswa.
.
Tuesday, May 31, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment