Birdman na Cash Money Records wamemfungulia mashitaka Jay Z na mtandao wake wa kusambaza nyimbo wa TIDAL.
Birdman na Cash Money Records wamefungua mashtaka ya kutaka walipwe kiasi cha dilla millioni 50 na kampuni ya Jay Z.TIDAL kufuatia kampuni hiyo kujihusiha na utoaji,usambazaji na uuzaji wa albamu ya Lil Wayne, Free Weezy Album.
Baada ya kupata taarifa ya kufunguliwa mashtaka na madai,wasemaji wa kampuni hiyo ya TIDAL wamesema walifanya kazi na Lil Wayne baada ya kukamilisha taratibu za makubaliano.
Cash Money wanadai bado Lil Wayne ni msanii ambaye anamkataba nao kuhusu shughulu zote za muziki hivyo ni kosa kufanya kazi nje ya makubaliano na wamepeleaka madai hayo kisheria.
Lil Wayne alisaini na TIDAL mwezi June.
0 comments:
Post a Comment