Gazeti la New York Post, limeandika,muimbaji Rihanna alikuwa katika maongezi kwa takribani miezi saba na wamiliki wa bidhaa za Samsung.
Meneja wa Jay Z na Rihanna, Jay Brown amesaidia Rihanna kukamilisha dili hilo.Mwanzoni mwa mwezi huu rapa Jay Z alipigwa picha akitoka katika jengo la Samsung na minongono ikaanza labda anataka kuiungia nao dili la kampuni yake ya kuuza na kusambaza muziki ya TIDAL,lakini badaye ikajulikana alikuwa akikamilisha dili la Rihanna.
Samsung watashiriki na Rihanna katika kuzitangaza bidhaa za Samsung Galaxy .
Ikumbukwe pia Roc Nation ina history nzuri ya kibiashara na kampuni ya Samsung kwani mwaka 2013 kampuni hiyo walishiriki kuipromotr albamu ya Jay Z Magna Carta… Holy Grail na walinunua nakala millioni moja.
Rihanna amepata dili hilo japo bado hajatangaza tarehe rasmi ya kuiachia albamu yake ya nane aliyoipa jina Anti japo ameahidi ataitoa kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Friday, October 30, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment