Chris Brown ametangaza kushinda kesi iliyokuwa ikimkabili kuhusu binti yake,Royalty kesi iliyofunguliwa na mama wa mtoto huyo,bi Nia Guzman.
Chris Brown na mama wa mtoto huyo,bi Nia Guzman juzi (May 24),walikuwa mahakamani kusikiliza kesi yao ambapo bi Guzman alifungua kesi akidai Brown si baba bora kwa binti yao kwani ana tabia za kihuni zikiwemo za kulipuliza mbele ya binti yao.
Jjai wa mahaka iliyokuwa ikiendesha kesi hiyo ameamua Breezy ataendelea kuwa na haki ya kuwa na biti yao huyo kwa siku 12 ndani yamwezi bila ya kuwa chini ya uangalizi.
Dai lingine la bi Guzman ni kuongezewa pesa za matumizi kutoka dola 2,500 ya sasa mpaka dola 16,000.
Hivi karibuni kulizuka sintofahamu baada ya mama wa Royalty kumvisha mtoto huyo mwenye miaka 2 kivazi kama msichan wa miaka 16.
0 comments:
Post a Comment